Hofu ya Ebola Nigeria, aliyekufa Calabar ashukiwa
Kwa sasa wataalamu wa afya nchini Nigeria wanazifanyia majaribio na utafiti sampuli za damu ya mtu huyo aliyeaga dunia. Siku ya Jumatano iliyopita Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza kuwa, nchi tatu zilizokuwa zimeathiriwa kwa kiasi kikubwa na ugonjwa huo ambazo ni Guinea, Sierra Leone na Liberia, zimeweza kuwa na wiki yake ya kwanza bila kuwa na kesi yoyote ya maambukizi ya ugonjwa wa Ebola tokea mlipuko wa ugonjwa huo uanze mwezi Machi mwaka 2014. Zaidi ya watu elfu kumi na moja walifariki dunia kwa ugonjwa huo wengi wao wakiwa ni kutoka katika nchi hizo tatu za magharibi mwa Afrika.
chanzo-tehran radio
Labels
AFRIKA
Post A Comment
Hakuna maoni :