
Wanamgambo wa kitakfiri wa al Shabab wameuteka mji mwingine katikati
mwa Somalia kufuatia kuondoka katika eneo hilo vikosi vya kulinda amani
vya Umoja wa Afrika nchini Somalia(AMISOM). Sheikh Abdiasis Abu Musab
Msemaji wa al Shabab amesema kuwa wameuteka mji wa Buqda kwa amani.
Wanajeshi wa AMISOM ambao waliuteka mji wa Buqda kutoka kwa wanamgambo
wa al Shabab katika kipindi cha chini ya mwezi mmoja uliopita,
waliondoka katika mji huo juzi usiku. Kwa upande wake afisa wa ngazi ya
juu wa jeshi la Somalia amesema kuwa wanajeshi wa AMISOM waliondoka
katika mji huo ili kukabiliana na al Shabab katika maeneo mengine na
kwamba watarudi huko baadaye.
Huu ni mji wa tatu kuanguka mikononi mwa wanamgambo wa kitakfiri wa al Shabab tangu Ijumaa
(tehranradio)
Post A Comment
Hakuna maoni :