HOT NEWS
Breaking news
Inaendeshwa na Blogger.

athumani matata

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *

Wanaofuata

Subscribe

Total Pageviews

Google Plus Card Widget

Google Plus Card Widget
Enjoy sport news

Auto Fb Page Inviter Script

Auto Fb Page Inviter Script
Hot news blog

Translate

slider1

technology

HII NI HATUA NYENGINE tangu wanafunzi 43 kutoweka Mexico Mwaka 1 upite.


 
Maelfu ya watu wamejitokeza kuishinikiza serikali kutoa ukweli kuhusu vifo vya wanafunzi 43
Mwaka mmoja uliopita, wanafunzi 43 walipotea katika mji wa Iguala katika jimbo la Guerrero, kusini mwa Mexican.
Maelfu ya watu wanashiriki katika maandamano makubwa katika mji mkuu wa Mexico kuadhimisho mwaka mmoja tangu kutokea kwa kisa hicho.
Uchunguzi wa serikali ulidai kuwa, wanafunzi hao walikabidhiwa kwa genge moja la uhalifu, ambao waliwauwa na kisha kuteketezwa mabaki ya maiti yao katika eneo la urushwaji taka.
Mwaka 1 tangu wanafunzi 43 kutoweka Mexico
Ripoti hiyo haijakataliwa tu na jamaa ya wanafunzi hao, bali pia ripoti kutoka kwa kundi moja la wataalamu wa uchunguzi huru, hivi majuzi ilihoji uhalali wa ripoti hiyo ya uchunguzi wa serikali.
Bernardo Santos Campos, babake Hose Angel, Ameiambia BBC kuwa wazazi wa wanafunzi hao waliotoweka hawatasitisha maandamano kamwe, hadi watakapojua kilichofanyika.
 
Kesi hiyo ni nembo ya kutoweka kwa maelfu ya raia wa Mexico
Rais wa Mexico Enrique Pena Nieto, ameahidi uchunguzi upya ufanywe.
Kesi hiyo ni nembo ya kutoweka kwa maelfu ya raia wa Mexico, ambao wametoweka katika muongo mmoja wa ghasia inayohusisha makundi hasimu ya ulanguzi wa dawa za kulevya na walinda usalama.

chanzo-bbcswahili.com
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :