technology

Muhuri, Haki Afrika zapinga kushirikiana na magaidi

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/6b3c53ee13e2c78a504eadfd4af626aa_XL.jpg
Mashirika ya kutetea haki za binadamu ya Muslims for Human Rights (MUHURI) na HAKI AFRIKA yenye makao yao mjini Mombasa, Kenya, yamesema kuwa serikali ya nchi hiyo inaendesha vita vya wazi dhidi ya Waislamu kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi. Tamko hilo la mashirika hayo ni radiamali kwa hatua ya serikali ya kutangaza kuyapiga marufuku mashirika hayo yasiyo ya kiserikali kwa tuhuma za kuwa na mfungamano na makundi ya kigaidi. Mkuu wa Haki Afrika, Hussein Khalid na mwenzake wa MUHURI, Khelef Khalifa wamesema mashirika yao yamepigwa marufuku kutokana na kusimamia haki na ukweli na kuikosoa serikali kila mara inapowakandamiza raia. Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana na leo, viongozi wa mashirika hayo mawili wamesema ripoti zao za mara kwa mara zinazoanika ukandamizaji wa polisi dhidi ya washukiwa wa ugaidi ndizo zilizoikasirisha serikali na kusababisha mashirika yao kupigwa marufuku. Wamesema hawaungi mkono ugaidi wala hawana uhusiano wowote na makundi ya kigaidi lakini wametaka serikali kuwatendea haki washukiwa wa ugaidi wanapokamatwa ili kudhihirisha kuwa Kenya ni nchi inayoheshimu utawala wa sheria.
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :