technology

Ulaya kugawana wakimbizi 120,000

Viongozi wa Ufaransa na Ujerumani wameahidi kutumia mfumo mpya ya kugawana wakimbizi baina ya nchi za muungano wa ulaya.
Tangazo hilo lilitolewa na rais wa Ufaransa Francois Hollande, ambaye alisema kuwa nchi yake itawachukua wakimbizi 24,000.
Amesema kuwa chini ya mipango huo kutoka kwa tume ya ulaya, jumla ya wahamiaji 120,000 watagawanywa baina ya nchi za muungano wa ulaya.
Image copyright AFP
Image caption Ufaransa imesema itawachukua wakimbizi 24,000
Chansela wa Ujerumani Angela Merkel anasema kuwa nchi yake pekee haiwezi kusuluhisha hali iliyopo kwa sasa.
Hata hivyo waziri mkuu wa Hungary Viktor Orban ameonya kuwa ugavi wa wahamiaji hauweza kufaulu chini ya mfumo wa sasa wa ulaya.
Image copyright Reuters
Image caption Ulaya kugawana wakimbizi 120,000
Wahamiaji elfu 20 wanakadiriwa kuingia Ujerumani mwishoni mwa juma na wengine wapatao elfu kumi na moja wanatarajiwa kufika nchini humo hii leo
Wakati huo huo Wahamiaji hawa kutoka Syria wamelalamikia hali duni katika kambi za wahamiaji nchini Hungary

bbcswahili.com
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :