Viongozi wa Ufaransa na Ujerumani wameahidi kutumia mfumo mpya ya kugawana wakimbizi baina ya nchi za muungano wa ulaya.
Tangazo hilo lilitolewa na rais wa Ufaransa Francois Hollande, ambaye alisema kuwa nchi yake itawachukua wakimbizi 24,000.
Amesema
kuwa chini ya mipango huo kutoka kwa tume ya ulaya, jumla ya wahamiaji
120,000 watagawanywa baina ya nchi za muungano wa ulaya. Image copyrightAFPImage caption
Ufaransa imesema itawachukua wakimbizi 24,000
Chansela wa Ujerumani Angela Merkel anasema kuwa nchi yake pekee haiwezi kusuluhisha hali iliyopo kwa sasa.
Hata hivyo waziri mkuu wa Hungary Viktor Orban ameonya kuwa ugavi wa wahamiaji hauweza kufaulu chini ya mfumo wa sasa wa ulaya. Image copyrightReutersImage caption
Ulaya kugawana wakimbizi 120,000
Wahamiaji elfu 20 wanakadiriwa kuingia Ujerumani
mwishoni mwa juma na wengine wapatao elfu kumi na moja wanatarajiwa
kufika nchini humo hii leo
Wakati huo huo Wahamiaji hawa kutoka Syria wamelalamikia hali duni katika kambi za wahamiaji nchini Hungary
NI MWANDISHI WA TOP NEWS BLOG, AMESHAFANYA KAZI YA UANDISHI NA UTANGAZAJI KATIKA KITUO CHA RADIO-PANGANI FM RADIO,LAKINI KWA SASA ANAENDELEA NA ELIMU YA JOURNALISM KATIKA NGAZI YA DIPLOMA-MUSLIM UNIVERSITY OF MOROGORO-TANZANIA
Post A Comment
Hakuna maoni :