technology

Saudia yaendelea kuishambulia Yemen; 19 wauawa

Saudia yaendelea kuishambulia Yemen; 19 wauawaKwa uchache raia 19 wa Yemen wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa katika mashambulio mapya ya anga ya Saudia katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Ripoti kutoka nchini Yemen zinasema kuwa, watu 6 wa familia moja wameuawa baada ya ndege za kijeshi za Saudia kufanya mashambulio katika nyumba moja kaskazini magharibi mwa jimbo la Sa'ada. Taarifa zaidi zinasema kuwa, tangu asubuhi ya leo mji wa Sa'ada kwa uchache umeshambuliwa mara 21. Raia wengine wa Yemen wameuawa leo katika mji wa Hajjah kufuatia mashambulio mengine ya anga ya Saudia. Mashambulio ya kinyama ya Saudia nchini Yemen yameendelea kusababisha mauaji kwa raia wasio na hatia na uharibifu mkubwa kwa nchi hiyo ambayo kwa sasa inakabiliwa na hali mbaya ya kibinadamu.
Hadi sasa watu wasiopungua 3000 wameuawa tangu Riyadh ilipoivamia na kuanza kufanya mashambulizi ya kinyama dhidi ya Yemen tarehe 26 Machi mwaka huu. Mashirika ya misaada ya kibinadamu yameendelea kutoa tahadhari kuhusiana na hali mbaya ya kibinadamu inayoikabili nchi hiyo.
(chanzo tehran idhaa ya kiswahili) http://kiswahili.irib.ir/habari/uadui/item/50164-raia-19-wa-yemen-wauawa-katika-mashambulio-ya-saudia
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :