technology

Saudi Arabia yashambulia kituo cha jeshi Yemen

Saudi Arabia yashambulia kituo cha jeshi Yemen Zaidi ya wanajeshi 40 wa Yemen wameuawa kufuatia shambulio la anga la Saudi Arabia dhidi ya kituo kimoja cha jeshi katika mji wa Hadhramaut katikati mwa nchi hiyo.  Aidha vyombo vya habari vya Yemen vimeripoti kuwa, zaidi ya wanajeshi 200 wa Saudia wamejeruhiwa katika shambulio hilo. Wakati huo huo vikosi vya Yemen vikisaidiwa na kamati za wapiganaji za wananachi limerusha makombora na kukilenga kituo cha kijeshi cha vikosi vya Saudia katika mji wa Dhahran al-Janub na kuvisababishia vikosi hivyo hasara kubwa. Hayo yanajiri katika hali ambayo, hali ya kibinadamu nchini Yemen inaripotiwa kuwa mbaya mno hasa katika kipindi hiki cha funga ya mwezi Mtukufu wa Ramadhani kutokana na kukosekana huduma na mahitaji muhimu ya maisha.  Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, zaidi ya Wayemeni 3,000 wameuawa  na wengine zaidi ya 14,000 wamejeruhiwa tangu Saudi Arabia ilipoanzisha mashambulizi yake ya kichokozi nchini humo miezi mitatu

Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :