Obama aikabidhi Kongres mapatano ya nyuklia ya Iran

Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel ameitaka Congress ya Marekani kuyakataa makubaliano hayo. Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry amemjibu Netanyahu kwa njia isiyo ya moja kwa moja akisema wanaopinga makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na 5+1 wanaishi katika ulimwengu wa ndoto.
Huku hayo yakijiri na katika kile kinachoonekana kama hatua za awali za nchi za Ulaya kujipanga kurudisha uwekezaji hapa Iran, Waziri wa Uchumi wa Ujerumani, Sigmar Gabriel, amewasili mjini Tehran akiongoza ujumbe wa ngazi za juu wa wanabiashara ambapo anatarajiwa kukutana na viongozi mbalimbali na wanabiashara wakubwa nchini hapa.
(chanzo tehran radio)
Post A Comment
Hakuna maoni :