technology

Marekani yakosolewa kwa kutokabiliana na Daesh

Marekani yakosolewa kwa kutokabiliana na DaeshSeneta John McCain wa jimbo la Arizona nchini Marekani ameikosoa vikali serikali ya Rais Barack Obama wa nchi hiyo kwa kushindwa kukabiliana na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh. McCain amesema kuwa mashambulio ya ndege za kivita za Marekani dhidi ya kundi hilo hayajakuwa na athari yoyote ya maana katika kudhoofisha na kulitokomeza kundi hilo linaloendelea kufanya uharibifu na mauaji makubwa katika nchi za Kiislamu. Ameongeza kuwa licha ya kuwa Marekani inadhibiti anga ya maeneo yanayoshikiliwa na kundi hilo la kitakfiri na Kizayuni, lakini kundi hilo linaendelea kukwepa mashambulio hayo ya Marekani na kudumisha shughuli zake za kuwasajili wanachama zaidi kupitia mitandao ya kijamii kwa kujificha katika maeneo ya mijini.
McCain amesema Marekani inapasa kuongeza juhudi zake za kuyaelimisha makabila ya Kisuni na askari usalama wa Iraq pamoja na wapinzani wa Syria ili eti kupata matokeo ya kuridhisha katika mapambano yake dhidi ya Daesh. Akizungumza hapo jana Jumatatu, Rais Obama alisema kuwa Washington kwa sasa haina mpango wowote wa kutuma askari zaidi nje ya nchi na kwamba inakusudia kuharakisha mwenendo wa kuipa Iraq silaha za kulenga vifaru.
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :