technology

Bunge la Misri: Watu 7, 000 wameuawa na polisi

Bunge la Misri: Watu 7, 000 wameuawa na polisiBunge la Misri limeonyesha wasi wasi wake kutokana na kushadidi hali ya ukandamizaji wa haki za binaadamu na kuzorota uchumi katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Ripoti iliyoandaliwa na bunge la Misri kuhusiana na hali ya haki za binaadamu na kadhalika hali ya uchumi wa nchi hiyo, ilikusanywa tangu kulipojiri mapinduzi ya kijeshi dhidi ya aliyekuwa rais wa taifa hilo Muhammad Mursi. Aidha ripoti hiyo imeelezea mauaji ya zaidi ya watu 7,000 katika maandamano dhidi ya serikali, huku zaidi ya watu elfu 50, wakiwamo wanaharakati wa kisiasa na haki za binaadamu wapatao 236 wakiwa wametiwa mbaroni kwa makosa tofauti na polisi ya nchi hiyo. Ripoti hiyo pia imeongeza kuwa, katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, Misri imeshuhudia ukandamizaji wa kupindukia wa haki za wanawake, watoto na wanafunzi huku mali za wapinzani 902, zikifilisiwa. Aidha imeongeza kuwa, katika kipindi cha miaka miwili hiyo, jumla ya taasisi 1096, mashirika 532, shule 82 na hospitali na vituo vya afya 28, vilisimamishwa na serikali ya Cairo. Kama hiyo haitoshi, serikali ya nchi hiyo imekuwa ikitekeleza ukandamizaji wa kupindukia dhidi ya uhuru wa kujieleza kwa kuzuia vyombo vya habari na mikusanyiko ya kisiasa. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, wanahabari wasiopungua 10 waliuawa huku kanali nne za televisheni zikifungwa. Aidha imeelezea kufungwa ofisi 12 za upashaji habari, kuwaacha bila ajira wanahabari 30, kutiwa mbaroni waandishi wengine wa habari wasiopungua 150 na kuripotiwa kesi 150 za ukandamizaji dhidi ya vyombo vya habari.
chanzo(tehran radio idhaa ya kiswahili)
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :