Duru rasmi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jana ziliripoti
habari ya kuuawa watu kadhaa katika mapigano na ghasia mashariki mwa
nchi hiyo. Duru ya usalama katika mkoa ulioathiriwa na machafuko wa Kivu
ya Kaskazini mashariki mwa Kongo imetangaza kuwa watu wasiopungua
watatu wameuawa kwenye mapigano hayo na makumi ya wengine kujeruhiwa na
kwamba uchunguzi umeanzishwa ili kuwasaka wahusika wa mauaji hayo.
Itakumbukwa kuwa watu watano waliuliwa na wengine 22 kujeruhiwa katika
mapigano yaliyotokea tarehe 24 Aprili mwaka huu katika mkoa wa Kivu ya
Kaskazini. Mauaji hayo yanajiri mkoani humo huku hali ya usalama ikizidi
kuzorota huko Kivu ya Kaskazini. Wiki iliyopita pia wanajeshi wawili wa
kulinda amani na raia wawili waliuawa katika mkoa huo katika shambulizi
la kuvizia la waasi wa Uganda.
Post A Comment
Hakuna maoni :