technology

Wapelekaji misaada kwa Boko Haram wanaswa

Wapelekaji misaada kwa Boko Haram wanaswa Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa limewatia mbaroni watu kadhaa katika jimbo la kaskazini mashariki la Yobe ambao walikuwa wakisafirisha mafuta kuwapelekea wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram. Taarifa iliyotolewa na jeshi la Nigeria imeeleza kuwa kufuatia maagizo yaliyotolewa kwa vikosi vya jeshi hilo ya kuchunguza madereva na magari ya mizigo, askari wa divisheni ya tatu ya jeshi wamewatia nguvuni baadhi ya vigogo na watu wanaowapatia misaada magaidi wa Boko Haram na kuwanasa pia wakiwa na dawa za kulevya na mada nyengine za kutia nishai. Taarifa hiyo imeongeza kuwa watu hao walikamatwa jana katika eneo lililoko baina ya miji ya Depchi na Gaidam, kilomita 70 kusini mwa Damaturu, makao makuu ya jimbo la Yobe. Hata hivyo taarifa hiyo haikueleza ni watu wangapi waliotiwa nguvuni katika operesheni hiyo. Jana hiyohiyo pia jeshi la Nigeria lilipiga marufuku utumiaji farasi katika jimbo la kaskazini mashariki la Borno katika jitihada za kukomesha mashambulio hatari ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram. Msemaji wa Jeshi katika jimbo la Borno Kanali Tukur Gusau amesema hatua hiyo imechukuliwa ili kuzuia mashambulio ya wanamgambo wa Boko Haram katika maeneo ya mbali katika jimbo hilo. Licha ya hatua kadhaa zilizochukuliwa na Rais Muhammadu Buhari tangu alipoingia madarakani mwishoni mwa mwezi wa Mei kwa lengo la kulisambaratisha kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram, mashambulio ya kundi hilo yangali yamepamba moto ambapo kwa mujibu wa vyombo vya habari watu wasiopungua 1,000 wameuawa katika wimbi la mashambulio yaliyofanywa na Boko Haram ndani ya muda wa chini ya miezi mitatu…/

(tehranradio)
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :