USIPITWE NA HII MTU WANGU !!!!!!!Waziri mkuu Australia apokonywa uongozi
Australia itapata waziri mkuu mpya baada ya Tony Abbott kuondolewa uongozini chama cha Liberal na waziri Malcolm Turnbull.
Kwenye
uchaguzi wa kiongozi wa chama uliofanywa haraka, Bw Abbott, ambaye
umaarufu wake umekuwa ukididimia kwa mujibu wa kura za maoni, alipata
kura 44 dhidi ya Bw Turnbull akipata kura 54.
Wabunge wa chama hicho hata hivyo walimpigia kura Julie Bishop kusalia kama naibu kiongozi wa chama hicho.
Bw Turnbull anatarajiwa kuapishwa baada ya Bw Abbott kumwandikia gavana mkuu na kujiuzulu.
Mapema
Jumatatu, kwenye kikao na wanahabari Canberra, Bw Turnbull alisema
iwapo Bw Abbott angesalia kiongozi wa chama hicho, serikali ya muungano
ingeshindwa kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Alisema ilikuwa vigumu
kwake kufanya uamuzi huo, lakini kwamba ni “wazi kuwa serikali
haijafanikiwa katika kutoa uongozi wa kiuchumi unaohitajika” na kwamba
Australia inahitaji mtindo mpya wa uongozi.
Bw Turnbull atakuwa waziri mkuu wa nne wa Australia tangu 2013.
Waziri
mkuu wa chama cha Leba Julia Gillard aliondolewa uongozini na Kevin
Rudd kwenye kura ya uongozi wa chama Juni 2013, miezi kadha kabla ya
uchaguzi mkuu ambao chama cha Liberal, chake Tony Abbott, kilishinda.
Bi Gillard mwenyewe alikuwa amemuondoa Rudd kama waziri mkuu 2010.
chanzo-bbc swahili.com
Post A Comment
Hakuna maoni :