
Vikosi vya jeshi la Syria vikiungwa mkono na harakati ya Muqawama
ya Lebanon Hizbullah vimewazingira magaidi katika mji wa kistratejia wa
Zabadani kusini magharibi mwa Syria. Habari zinasema kuwa vikosi vya
Syria na vile vya harakati ya Muqawama ya Lebanon vimesonga mbele katika
mji huo na kuudhibiti msikiti wa al Jasr na majengo mengine yaliyo
karibu. Magaidi kadhaa wameuawa katika mapambano kati yao na vikosi vya
Syria na wanamuqawama wa Lebanon, na kufanikiwa kuangamiza mada za
miripuko zilizokuwa zimetegwa na magaidi ndani ya msikiti wa al Jisr.
Mji wa kistratejia wa Zabadani unaopatikana katika mkoa wa Rif Dimashq
umekuwa ukitumiwa kama ngome ya makundi ya kigaidi.
chanzo-tehran radio
Post A Comment
Hakuna maoni :