technology

HALI MBAYA YA USAFI WA FUKWE TANGA



Wananchi wa kijiji cha kipumbwi wilayani pangani wametakiwa kutotupa taka katika fukwe za bahari ya hindi na kushiriki katika kusafisha mazingira ya bahari kwa ujumla.

Akiongea na TOP NEWS BLOG katibu wa BMU MUSA OMARI MASUDI kijiji cha kipumbwi, katika mkutano ulio itishwa na shirika lisilo la kiserikali la SEA SENSE, ametoa wito kwa wananchi wa kipumbwi kuacha tabia hiyo kwani inasababisha mripuko wa magonjwa,na kupelekea vifo kwa viumbe walioko baharini.


Na kwaupande wake mwenyekiti wa kitongoji HASANI MUHAMMEDI amewataka wakazi wa kipumbwi kuona umuhimu wa kusafisha mazingira ya BAHARI na FUKWE na suala la kusafisha ufukwe na la watu wote na sio BMU peke yao.

Hayo yamejiri jana katika mkutano uliotishwa na shirika la SEA SENSE linalo toa elimu juu ya uhifadhi wa mazingira BAHARI, FUKWE na  kupiga vita uvuvi haramu katika WILAYA ya PANGANI





Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :