technology

WHO yawaenzi wahudumu wa afya kwenye Siku ya Kibinadamu

Katika kuelekea Siku ya Kibinadamu Duniani, Shirika la Afya Duniani, WHO, linamulika mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya wahudumu wa afya na miundombinu ya afya, ambayo Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo, Dkt. Margaret Chan, ametaja kuwa ni ukiukaji wa sheria ya kimataifa ya kibinadamu.
Katika mchakato wa kuwaenzi wahudumu wa afya, WHO itazindua kampeni kwenye intaneti ya kutambua juhudi za madaktari, wauguzi na wahudumu wengine, na kukumbusha nchi wanachama na pande kinzani katika mizozo kutimiza wajibu wao wa kuwalinda wahudumu wa afya na mfumo mzima wa huduma za afya.
Kampeni hiyo inalenga kumulika hatari zinazowakabili wahudumu wa afya na haja ya kuongeza juhudi za kuwalina.http://www.unmultimedia.org/radio/kiswahili/2015/08/who-yawaenzi-wahudumu-wa-afya-kwenye-siku-ya-kibinadamu/#.VdF30OLfrox
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :