
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim
Jong-un amevitaka vikosi vya mpakani vya nchi hiyo kujiweka katika
mazingira ya kuingia vitani wakati wowote. Kiongozi wa Korea Kaskazini
ametoa amri hiyo baada ya kushadidi hitilafu na mivutano kati ya nchi
yake na jirani yake Korea Kusini. Kim Jong-un aidha ametoa amri hiyo
ambayo inaanza kutekelezwa leo baada ya pande mbili kushambuliana kwa
mizinga katika maeneo wa mpaka wa nchi mbili hizo yenye ulinzi mkali.
Kiongozi wa Korea Kaskazini ameyataka majeshi ya nchi yake yaliyoko
mpaka kujiweka tayari kabisa na kujizatiti kwa silaha kwa ajili ya vita
itakapofika saa 11 jioni leo kwa majira ya nchi hiyo.
Korea Kusini nayo imeviweka tayari
vikosi vyake vya kijeshi baada ya muda ulioainishwa na Pyongyang kwa
Seoul ya kuondoa vipaza sauti vyake vya matangazo katika maeneo ya
mpakani. Jana Korea Kaskazini iliipatia Korea Kusini masaa 48 iwe
imezima vipaza sauti vyake vya matangazo na kwamba, itakabaliwa na
shambulio la kijeshi endapo haitafanya hivyo baada ya muda ulioainishwa
kumalizika.
(chanzo tehrani radio)
Post A Comment
Hakuna maoni :