technology

Nkurunziza ashinda uchaguzi wa rais Burundi

NkurunzizaTume ya Taifa ya Uchaguzi ya Burundi imetangaza Rais Pierre Nkurunziza kuwa mshindi wa kiti cha urais katika uchaguzi uliofanyika Jumanne iliyopita.  Tume ya uchaguzi imesema kuwa, Nkurunziza ameshinda kiti cha urais baada ya kujipatia asilimia 65.41 za kura. Uchaguzi huo ulifanyika Jumanne iliyopita licha ya kuweko malalamiko ya ndani na nje na hata miito ya kutaka kuakhirishwa uchaguzi huo. Hata siku moja kabla ya siku yenyewe ya kufanyika uchaguzi kulishuhudiwa matukio ya ukandamizaji wa vyombo vya usalama dhidi ya wapinzani na watu kadhaa kuuawa.
Nchi na taasisi nyingi duniani zilikataa kupeleka waangalizi kwenye uchaguzi huo. Wapinzani walikuwa wakipinga hatua ya Nkurunziza kugombea urais kwa mara ya tatu wakisema anaenda kinyume cha katiba na mapatano ya amani ya mwaka 2006 ya mjini Arusha Tanzania.
Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa vyama vyote nchini Burundi kuanza mara moja mazungumzo ya kisiasa kwa ajili ya kutatua hitilafu zao na kushughulikia changamoto zinazoikabili nchi hiyo.
(chanzo tehran radio)
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :