technology

Hatimaye Wapinzani Burundi wayakataa matoke ya uchaguzi

Wapinzani Burundi: Hatuyakubali matokeo ya uchaguziChama kikuu cha upinzani nchini Burundi kimetangaza rasmi kutoyatambua matokeo ya uchaguzi mkuu nchini humo, ambayo yamempa ushindi Rais Pierre Nkurunziza. Akiongea na waandishi wa habari Agathon Rwasa, Mkuu wa chama cha FNL nchini Burundi amesisitiza kuwa, chama chake hakiyatambui matokeo hayo ya uchaguzi wa tarehe 21. Rwasa ameutaja uchaguzi huo kuwa uliokosa itibari na hivyo ametaka kuitishwa uchaguzi mkuu mpya ambao utawashirikisha viongozi wa vyama vyote vya upinzani katika anga salama. Aidha Agathon Rwasa amepinga pendekezo la kuunda serikali ya umoja wa kitaifa, na kusisitiza kuwa, suala hilo litawezekana tu iwapo serikali ya sasa itaandaa uchaguzi wa wazi na ulio huru na wa kidemokrasia nchini. Licha ya kushadidi kwa wimbi la malalamiko ya ndani na nje yaliyomtaka Rais Pierre Nkurunziza kuachana na azma yake ya kugombea muhula wa tatu katika uchaguzi mkuu, lakini rais huyo alipuuza malalamiko hayo na kushiriki katika uchaguzi wa tarehe 21 mwezi huu ambapo aliibuka kuwa mshindi. Kwa mujibu wa matokeo rasmi, Rais Nkurunziza ameshinda kwa kujizolea asilimia 69.41 ya kura zilizopigwa huku Agathon Rwasa wa FNL akishikilia nafasi ya pili kwa asilimia 19 ya kura hizo.

(chanzo tehran radio)
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :