
Binti mdogo aliyekuwa na umri wa miaka 10 na ajuza mmoja siku ya Ijumaa
walitekeleza mashambulio ya kigaidi kwa kujilipua huko kaskazini
mashariki mwa Nigeria na kuuwa makumi ya watu. Kanali Sani Usman msemaji
wa jeshi la nchi hiyo amesema kuwa mlipuko huo wa kigaidi uliotokea
katika soko la mji wa Gombe ulioko kaskazini mashariki mwa Nigeria
ulitekelezwa na binti aliyekuwa na umri wa miaka 10 na ajuza mmoja ambao
wote ni wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Boko Haram. Awali
maafisa wa nchi hiyo walitangaza kuwa milipuko miwili ya kigaidi
ilikuwa imetokea katika eneo hilo na kusababisha maafa ya watu 50 na
kujeruhi wengine 70. Tokea kuingia madarakani Rais Muhammad Buhari wa
Nigeria na kuahidi kupambana vilivyo na Boko Haram, kundi hilo
limezidisha operesheni zake za kigaidi nchini humo ambapo mamia ya watu
wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
(CHANZO tehran radio )
Post A Comment
Hakuna maoni :