technology

CNN yafichua namna US inavyowapa mafunzo Daesh

CNN yafichua namna US inavyowapa mafunzo Daesh
Televisheni ya Marekani ya CNN imefichua habari inayosema kuwa, Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo imewapa mafunzo magaidi wa Daesh. Televisheni hiyo ya Marekani imesambaza mkanda wa video kupitia Intaneti ambapo ndani ya mkanda huo anaonekana Kanali Gulmurod Khalimov, mkuu wa zamani wa jeshi la polisi la Tajikistan ambaye hivi sasa amejiunga na kundi la kigaidi la Daesh akisema kuwa, yeye binafsi ameshiriki mara tatu katika mafunzo ya kijeshi ndani ya ardhi ya Marekani na moja ya mafunzo hayo ameyapata kwenye jimbo la Louisiana la Marekani. Hata Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imekiri jambo hilo. Msemaji mmoja wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ameiambia televisheni ya CNN kwamba Kanali Khalimov alipata mafunzo ya kijeshi katika vipindi vitano tofauti nchini Marekani na Tajikistan baina ya mwaka 2003 hadi 2014. Amesema, mafunzo hayo yalitolewa na kusimamiwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kwa kile alichodai ni kupambana na ugaidi. Licha ya viongozi wa Marekani kukiri mara kwa mara kuwa ndio waliolianzisha na kulipa mafunzo kundi la kigaidi la Daesh lakini hivi sasa wameunda muungano wa kulipiga vita kundi hilo. Wachambuzi wa mambo wanasema kuwa, huo ni mchezo wa kisiasa tu wa Marekani, na kwamba Washington na waitifaki wake hawana nia ya kweli ya kupambana na kundi hilo la kigaidi
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :