technology

Yemen wamiminika barabarani kulaani jinai za Saudia

Wananchi wa Yemen wamefanya maandamano makubwa mjini Sana'a kulalamikia mashambulizi ya kinyama ya Saudia dhidi ya nchi yao. Maandamano hayo makubwa yamefanyika baada ya kiongozi wa harakati ya Ansarullah, Sayyid Abdul Malik al Houthi kutoa mwito kwa wananchi hao kujitokeza kwa wingi kwenye maandamano kulaani jinai za Saudi Arabia dhidi ya nchi yao. 

Katika hotuba yake aliyoitoa kwa njia ya televisheni, al Houthi amesema kuwa, utawala wa ukoo wa Aal Saud wa Saudi Arabia unafanya jinai zilezile zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi madhlumu wa Palestina. Sayyid Abdul Malik al Houthi ametoa hotuba hiyo kuadhimisha mwaka wa kwanza tangu yalipofanyika mapinduzi ya wananchi nchini Yemen na kusema kuwa, adui Mzayuni asingelithubutu kukivunjia heshima kibla cha kwanza cha Waislamu yaani Masjidul Aqsa, kama si uadui wa Saudia dhidi ya wananchi wa Yemen. Amesema ukoo wa Aal Saud unashirikiana na Israel katika mambo mengi ikiwa ni pamoja na kuuzamisha umma wa Kiislamu kwenye dimbwi la matatizo na fitna za kitaifa, ili Waislamu wasifikirie kabisa suala la kukomboa kibla chao cha kwanza huko Palestina kutoka katika makucha ya utawala ghasibu wa Kizayuni. Amesema Saudi Arabia inashirikiana na Israel kulitumbukia eneo hili kwenye vita na kwamba anayefaidika pekee kwenye machafuko na vita hivyo ni utawala wa Kizayuni wa Israel.
chanzo-http://kiswahili.irib.ir/habari
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :