technology

USIKOSE HII ,,,,NAM yaunga mkono miradi ya nyuklia ya Iran

NAM yaunga mkono miradi ya nyuklia ya IranHarakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM) imesema inaunga mkono miradi ya nyuklia ya Iran ikiwemo haki ya Tehran ya kurutubisha madini ya urani. Taarifa iliyotolewa jana kwenye kikao cha mwezi huu cha Bodi ya Magavana ya wakala wa IAEA na Reza Najafi Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika wakala huo imetilia mkazo misimamo mikuu ya harakati ya NAM, ikiwemo haki muhimu na isiyoweza kutenganishwa ya nchi zote duniani ya kustafidi na nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani na kueleza kuwa: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina haki ya kutumia teknolijia ya nyuklia kwa malengo ya amani. Taarifa iliyotolewa Reza Najafi katika kikao cha Bodi ya Magavana ya IAEA imeongeza kuwa: Harakati ya NAM imepokea vizuri makubaliano yaliyofikiwa kati ya Iran na kundi la 5+1 na inaamini kuwa makubaliano hayo yatasaidia kutatua kwa amani kadhia ya nyuklia ya Iran.

(Tehran radio)
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :