technology

KUTUMIKISHWA KWA WATOTO KATIKA SHUHULI ZA UVUVI TANGA BADO CHANGAMOTO...........



Tatizo la kuwatumikisha watoto katika shughuli  ya uvuvi katika kijji cha kipumbwi wilayani pangani bado linaendelea hali inayo pelekea watoto hao kukosa elimu na kuhatarisha maisha yao.

Akiongea na PANGANI FM MMOJA  wa wananchi  katika mkutano ulioitishwa na SHIRIKA LISILO LA KISERIKALA  LA SEA SENSE linalo toa elimu juu ya uhifadhi wa  rasili mali bahari na utunzaji wa mazingira ,amesema hali hiyo ipo na inasababishwa na baadhi  ya familia kuwa na kipato kidogo hivyo wazazi kuwa achia watoto wao kwenda baharini.


Hata hivyo katibu wa BMU katika kijiji cha KIPUMBI ndugu MUSA OMARI MASUDI  amekiri  kuwepo kwa tatizo hilo  na kwa upande wake yeye amesema tatizo la watoto kwenda baharini lina sababishwa na  manahoza kuwatumia watoto hao kwa kuwalipa ujira mdogo.


Na kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji ndugu HASANI MUHAMMED amesema yeye anapata wasiwasi juu ya suala hili na amewataka manahodha kuacha tabia ya kuwatumikisha watoto katika uvuvi.


Tatizo la kutumikishwa kwa watoto katika kijiji cha kipumbwi katika uvuvi linaendelea kuchukua sura mpya kutokana na kijiji cha kipumbwi  kutokua na sheria yoyote ya kudhibiti suala hili la watoto wa shule za msingi na sekondari kutoka katika maeneo ya SAKURA,MTONGA,MAKARAWE na SANGE kwa ajili ya uvuvi.


Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :