technology

Kongamano la kukabiliana na ugaidi laanza Mauritania

Kongamano la kukabiliana na ugaidi laanza MauritaniaKongamano la kimataifa la kukabiliana na makundi yenye kufurutu ada limeanza nchini Mauritania. Kongamano hilo lililoanza jana Jumatano linafanyika mjini Nouakchott, mji mkuu wa nchi hiyo. Wasomi, watafiti na mahatibu kutoka nchini za Ulaya, eneo la Sahel mwa Afrika, Marekani na baadhi ya nchi za Kiafrika, wanahudhuria kongamano hilo la siku mbili na lililofunguliwa na Waziri Mkuu wa nchi hiyo Yahya Ould Hademine. Akihutubia kongamano hilo, Sheikh Abdallah bin Bayyah mmoja wa wasomi wakubwa wa Mauritania alizitaka nchi za dunia kutenga bajeti itakayodhamini mahitaji katika sekta ya utamaduni kwa lengo la kuwazuia vijana na wasichana kujiunga na makundi yenye kufurutu ada na ambayo yanatekeleza jinai dhidi ya binaadamu kwa jina la Uislamu. Aidha Sheikh Bin Bayyah amesema kuwa hii leo ulimwengu unahitajia sana kuliko wakati mwingine wowote, kuandaliwa mipango ya kiutamaduni na kiusalama sanjari na kufuatwa mwenendo wa mazungumzo ya usawa baina ya pande hasimu badala ya kufuata mwenendo wa mapigano na mauaji. Aidha washiriki wa kongamano hilo litakalomaliza shughuli zake hii leo, wamelaani jinai za makundi ya kigaidi na kitakfiri hususan Daesh, Boko Haram na Jab’hatu Nusra.

(chanzo tehran radio idhaa ya kiswahili.com)
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :