''Afadhali kufariki baharini badala ya kuishi Libya''

Miaka mitatu iliopita walitoka nchini Nigeria na kuelekea Libya kwenye harakati za kutafuta maisha mazuri.
Alianzisha saluni iliyowahudumia wenyeji na wahamiaji.

Walifungwa macho wakati wa safari yote kutoka Benghazi hadi Tripoli ambayo ni safari ya Zaidi ya Kilomita 1,000 bila chakula au maji kabla ya kukabidhiwa kwa timu nyingine ya kusafirisha wahamiaji ambayo iliwasafirisha kwa masaa manne na kuwapeleka katika sehemu moja ya pwani isio na watu.
Huko walikutana na mashua tatu za kusafirisha wahamiaji
Waliagizwa kuingia katika boti hiyo kabla ya wasafirishaji hao kuipeleka baharini nyakati za usiku.

Baada ya masaa kadhaa ya kusafiri kwenye bahari, mashua hiyo ilianza kuvuja. Wanawake walianza kulia na kila mtu alihofia kuwa ndio mwisho wao.
Kwa bahati nzuri walipatikana na chombo cha uvuvi ambacho kiliwaokoa na badaaye kutuma ujumbe kwa chombo cha usalma walinzi wa pwani ya Italy ambao walituma mashua ya MSF Dignity 1 kuwaokoa.
Wakati mashua hiyo iliporudi kutia nanga ilikua imebeba wahamiaji 316 kutoka maeneo tofauti ya usaidizi katika bahari ya shamu.

Walipowasili katika eneo la Vibo Valentia, katika pwani ya Kusini magharibi mwa Calabria nchini Italy, alisajiliwa na kutumwa hospitalini kufanyiwa ukaguzi wa kiafya .
Wanawake wengine wanne walijiunga naye ili kufanyiwa uchunguzi wa virusi vya HIV kwa kuwa walibakwa huko Libya.

Alipanda basi iliyokuwa ikielekea kusini mshariki mwa Italy akisubiri kuzaliwa kwa mwanawe Dignity.
(chanzo bbc swahili.com)
Post A Comment
Hakuna maoni :