technology

White House: Obama kutetea mashoga akiwa Kenya

White House: Obama kutetea mashoga akiwa KenyaHuku viongozi wa Kenya na makundi ya kiraia yakiendelea kumuonya Rais wa Marekani, Barack Obama, dhidi ya kuishinikiza nchi yao ikubali ndoa za watu wa jinsia moja wakati atakapokuwa Nairobi mwishoni mwa mwezi huu, ikulu ya White House mjini Washington imesisitiza kuwa, kiongozi huyo ataligusia suala hilo wakati wa ziara yake hiyo. Msemaji wa Rais Obama, Josh Earnest, amesema kiongozi huyo hatosita kuelezea mtazamo wake kuhusu suala la ushoga. Naibu Rais wa Kenya, William Ruto, Spika wa bunge la Kitaifa, Justin Muturi na mwenzake wa Seneti, Ekwe Ethuro ni miongoni mwa viongozi waandamizi wa Kenya ambao wamemuonya Obama dhidi ya kuishinikiza nchi yao kuwakubali mashoga. Makumi ya wabunge na mashirika mengi ya kiraia pia yanamtaka Obama kuheshimu utamaduni wa Wakenya na Waafrika na kujiepusha kuzungumzia suala hilo atakapoitembelea Kenya Julai 25. Spika wa bunge la kitaifa amesema bunge litachukua hatua iwapo Obama atadharau mila na utamaduni wa Wakenya
chanzo (tehran radio idhaa ya kiswahili)
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :