technology

MWINGEREZA AFELI MAJARIBIO AZAM FC,NAFASI YAKE KUCHUKULIWA NA MKENYA

Mambo yameshaharibika kwani lile dili la kiungo Ryan Burge kutaka kuwek a rekodi ya kuwa Muingereza wa pili kucheza Ligi Kuu Bara limeshindikana na muda wowote ataondoka nchini kurudi kwao.

Kally Ongala, ndiye raia wa kwanza wa Uingereza, kucheza Ligi Kuu Bara alipozichezea Yanga na Azam, kabla ya kuachana na soka na sasa ni kocha.
Burge alisema: “Mambo yameshindikana na nitarejea nyumbani ambako nimepata timu ya kuchezea, sijajua ni kitu gani kilichokwamisha usajili wangu.”
WANGA (MBELE) WAKATI AKIWA EL MERREIKH AKIPAMBANA NA MIGI WAKATI AKIICHEZEA 
Taarifa zinaeleza baada ya ujio wa Allan Wanga, Azam FC imeona ni vizuri kumchukua Mkenya huyo na kuachana na Mwingereza huyo.


Burge alisema: “Muda wowote nitaondoka kurejea nyumbani kwa sababu kuna timu imetokea kunihitaji, siwezi kukutajia ni timu gani mpaka nitakapofika huko na kufanya nao mazungumzo.”
chanzo salehjembe.blospot.com
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :