technology

Ombi la Unesco kwa ICC kuhusu uharibifu wa Timbuktu

Ombi la Unesco kwa ICC kuhusu uharibifu wa TimbuktuShirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (Unesco) limeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kuanzisha uchunguzi kuhusu kubomolewa na makundi ya wanamgambo makaburi ya kale huko kaskazini mwa Mali. Irina Bokova Mkurugenzi Mkuu wa Unesco amesema kuwa kuharibiwa urithi wa kiutamaduni kunachukuliwa kuwa ni jinai ya kivita kwa mujibu wa makubaliano ya The Hague ya Umoja wa Mataifa ya mwaka 1954. Mwaka 2012 wanamgambo wanaobeba silaha waliuteka mji wa Timbukutu yapata umbali wa kilomita 1000 kaskazini mashariki mwa mji mkuu wa Mali Bamako na kubomoa makaburi ya masharifu wa Kiislamu ya karne ya 15 na 16. Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Unesco amesema kuwa miezi miwili iliyopita alikutana na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa mahakama ya ICC na kwamba anaamini kuwa mahakama hiyo inafanya jitihada za kufanya uchunguzi kuhusu kuharibiwa urithi huo wa kitamaduni huko kaskazini mwa Mali na kesi hiyo kuanza kusikiliza mahakamani. Tawi la kiutamaduni la Umoja wa Mataifa limeanza kuujenga upya mji wa kihostoria wa Timbuktu unaojulikana kwa jina la mji wa watakatifu 333 kwa msaada wa serikali ya Mali na taasisi nyingine za kimataifa, baada ya wanamgambo wenye silaha kundoka mjini humo kufuatia oparesheni za kijeshi za mwaka 2013.

tehran radio idhaa ya kiswahili.com
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :