technology

Saudia inashambulia kwa silaha zilizopigwa marukufu

Saudia inashambulia kwa silaha zilizopigwa marukufu Shirika la Haki za Binadamu la Human Rights Watch (HRW) limesema kuwa, kuna ushahidi wa kutosha unaoonesha kuwa Saudi Arabia inaendelea kutumia mabomu yaliyopigwa marufuku kama vile ya vishada nchini Yemen na kuonya kuwa mashambulio hayo yanawaletea madhara makubwa raia.
Shirika hilo limetoa ripoti yake leo Jumapili baada ya maafisa wake kutembelea mkoa wa Sa’ada wa kaskazini mwa Yemen na kusema kuwa, Saudia imekuwa ikitumia mabomu ya vishada kuwalenga raia na maeneo ya makazi ya watu wa kawaida.
Shirika hilo lenye makao yake nchini Marekani limesema kuwa, Saudia imetumia aina tatu tofauti za mabomu yaliyopigwa marufuku ya vishada dhidi ya raia wa Yemen.
Shirika hilo limesambaza pia picha zinazoonesha mabaki ya mabomu ya vishada yaliyotumiwa na Saudia kwenye maeneo mbalimbali ya Yemen kama vile al Nushoor na al Maqash, mkoani Sa’ada, kaskazini mwa Yemen.
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :