technology

Al-Shabab waua watu wasiopungua 25 Somalia

Serikali ya Somalia imetangaza kuwa, kwa uchache watu 25 wameuawa baada ya wanamgambo wanaofungamana na mtandao wa al-Qaeda wa al-Shabab kufanya mashambulio mawili tofauti katika maeneo ya kusini mwa nchi hiyo.

Abdulkadir Mohamed Nur Siidii Gavana wa jimbo la Lower Shabelle amesema kuwa, kwa akali wanajeshi 15 na wanamgambo 10 wameuawa wakati kundi la wanamgambo wa al-Shabab waliposhambulia majengo ya wanajeshi katika miji ya Mubarak na Awdheegle. 

Mashuhuda wanasema kuwa, mamia ya askari wamepelekwa katika maeneo hayo kwa ajili ya kudhibiti hali ya mambo. 

Sheikh Abdiasis Abu Muscab msemaji wa kundi la kigaidi la wanamgambo wa al-Shabab amesema kuwa, wapiganaji wao ndio waliotekeleza shambulio hilo. 

Hayo yanajiri katika hali ambayo, askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika nchini Somalia, AMISOM wametangaza kuwa, wamefanikiwa kufelisha shambulizi la kigaidi la wanamgambo wa ash-Shabab nchini humo. Mmoja wa makamanda wa askari hao, amesema kuwa wanamgambo wa al- Shabab walijaribu kudhibiti kambi za jeshi la serikali kusini mwa Somalia, lakini askari wa AMISOM wakafanikiwa kuzima jaribio hilo
Post A Comment
  • Blogger Comment using Blogger
  • Facebook Comment using Facebook
  • Disqus Comment using Disqus

Hakuna maoni :